KUHUSU SHULE BORA

Kwa ufadhiri kutoka Serikali ya watu wa Uingereza(UK) kutoka 2021 hadi 2027, Programu ya Shule Bora kitaifa itafanya kazi kusaidia serikali katika programu ya mageuzi ya elimu, na kwa kuboresha elimu katika Serikali za Mitaa na shule za mikoa tisa ya Tanzania yenye changamoto nyingi. Takribani watoto milioni 4, watanufaika na hii programu, nusu yao wakiwa wasichana. Mageuzi na na uvumbuzi vitajaribiwa na kutathminiwa katika ngazi ya mtaa ili mbinu bora zilizothibitishwa ziweze kutumika katika shule zote za msingi nchini.

Kitaifa, Shule Bora hutoa msaada wa kitaalamu kwa serikali kuhusu na kwa programu ya pili ya elimu ya Lipwa Kwa Matokeo yani EpforR II inayofadhiriwa na na wadau mbalimbali. Katika EPforR II, malengo ya utendaji wa kitaifa yanafanyika kwa makubaliano ya pande zote mbiliserikali na wafadhili kuhusu malipo yanayotokana na na mafanikio lengwa. Hii huchochea mabadiliko ya kudumu ya kimfumo kama vile usawa wa usambazaji wa walimu na utoaji wa vitabu vya kiada.

Washirika wetu wakuu

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (MOEST) – Inatoa mwongozo wa kisera na uangalizi matokeo muhimu ya programu.

Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) – kusimamia utekelezaji katika Mikoa na Halmashauri.

Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE) – kutoa mafunzo endelevu ya kitaalamu yenye ubora juu kwa walimu.

Wakala wa Maendeleo ya Usimamizi wa Elimu (ADEM) – Kuboresha usimamizi wa elimu nchini Tanzania

Cambridge Education (CE) ni mshirika wa utoaji wa usaidizi wa kitaalamu kwa Shule Bora. Programu inatekelezwa na washirika wakuu wa Action on Disability and Development (ADD), Plan International, na International Rescue Committee (IRC), na washirika wengine.

Shule Bora imejikita katika matokeo manne;

  1. Kujifunza: Watoto wote wapo shuleni wanajifunza
  2. Kufundisha: UK aid inasaidia uimarishaji wa kufundisha kwa walimu wa
    Tanzania
  3. Jumuishi: Watoto wote wapo shuleni zenye mazingira salama, yanayovutia
    kujisomea na kuwawezesha kumaliza elimu msingi na kwendelea hadi sekondari
  4. Kujenga Mifumo: UK aid inasaidia Serikali kuimarisha thamani ya fedha
    zitolewazo kwa elimu shuleni katika ngazi za serikali za mitaa na kitaifa

Ili kufikia matokeo haya. Shule Bora inafanya kazi kutoa

Shule Bora imejikita katika matokeo makuu matano, kila moja ikilenga wadau muhimu tofauti katika kufanikisha matokeo ya programu

Ushirikishwaji wa Jamii

Kuhakikisha wazazi na jamii wanaunga mkono kikamilifu elimu kwa watoto wote na wanashiriki katika uboreshaji wa shule

Ufundishaji

Kuwapa walimu maarifa, msaada, na motisha ya kutoa elimu mjumuishi yenye ubora wa juu kwa wanafunzi wote.

Usimamizi na Usalama wa Shule

Kusaidia viongozi wa shule kuhakikisha shule zinaongozwa vyema, zinatoa umuishi, usalama na uziefu wa kukaribisha wanafunzi.

Msaada kwa Serikali za Mitaa

Kuhakikisha maafisa elimu wa Serikali za Mitaa wana ujuzi wa taarifa na taratibu za kusaidia shule kuweza kutoa mafunzo bora, salama na jumuishi.

Programu ya Elimu ya Lipwa Kwa Matokeo II (EPforR II) na Usaidizi wa Kitaifa

Kutoa msaada wa kitalaamu na mwongozo kwa maafisa wa elimu wa kitaifa ili kutoa motisha na kuboresha uimarishaji wa mfumo wa elimu, ikiwa ni pamoja na kupanga, matumizi ya takwimu na usimamizi wa utendaji.